Verse 1
Pasipo makosa Mkombozi wetu,
Katika baraza la wakosefu
Na wote walia asulibiwe,
Aachwe Baraba na Yesu afe
Aachwe Baraba na Yesu afe
Verse 2
Ee Yesu washika msalaba wako,
Na unakubali kufa juu yake
Ee Yesu useme sababu gani,
Ya nini mateso makali hayo?
Ya nini mateso makali hayo?
Verse 3
Ni pendo kwa Baba wa uwinguni,
Ni huruma yangu kwa wakosefu.
Ewe mkristu kumbuka mateso yangu,
Uache makosa, uache dhambi
Uache makosa, uache dhambi
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.