SectionsEntrancePasipo Makosa

Pasipo Makosa

LentEntrance
Verse 1

Pasipo makosa Mkombozi wetu,

Katika baraza la wakosefu

Na wote walia asulibiwe,

Aachwe Baraba na Yesu afe

Aachwe Baraba na Yesu afe

Verse 2

Ee Yesu washika msalaba wako,

Na unakubali kufa juu yake

Ee Yesu useme sababu gani,

Ya nini mateso makali hayo?

Ya nini mateso makali hayo?

Verse 3

Ni pendo kwa Baba wa uwinguni,

Ni huruma yangu kwa wakosefu.

Ewe mkristu kumbuka mateso yangu,

Uache makosa, uache dhambi

Uache makosa, uache dhambi

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.