Bwana ndiye fungu la posho langu,
Na la kikombe changun{Wewe unaishika kula yangu,
Nimemwambia Bwana, Bwana
Wewe ndiwe Bwana wangu } *2
Nitamhimidi Bwana aliyenipa shauri
Na mtima wangu, umenifundisha usiku
Nimemweka Bwana mbele yangu daima
Kwa kuwa yuko kuumeni kwangu sitaondoshwa
Kwa hivyo moyo wangu, unafurahi moyo wangu
Washangilia, nao mwili wangu utakaa
Kwa kutumaini, Maana wewe Bwana
Hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu
Utanijulisha njia, njia ya uzima
Mbele ya uso wako, ziko furaha tele,
Na katika mkono wako wa kuume
Mkono wa kuume mna neema ya milele
Mungu nihifadhi mimi, maana nakukimbilia
Wewe Mungu wangu, Bwana ndiwe Bwana wangu,
Wewe Bwana ndiwe fungu la posho langu
Na la kikombe changu wewe unaishika kula yangu
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.