Posho Langu

Marian,Ordinary TimeEucharist
Chorus

Bwana ndiye fungu la posho langu,

Na la kikombe changun{Wewe unaishika kula yangu,

Nimemwambia Bwana, Bwana

Wewe ndiwe Bwana wangu } *2

Verse 2

Nitamhimidi Bwana aliyenipa shauri

Na mtima wangu, umenifundisha usiku

Nimemweka Bwana mbele yangu daima

Kwa kuwa yuko kuumeni kwangu sitaondoshwa

Verse 3

Kwa hivyo moyo wangu, unafurahi moyo wangu

Washangilia, nao mwili wangu utakaa

Kwa kutumaini, Maana wewe Bwana

Hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu

Verse 4

Utanijulisha njia, njia ya uzima

Mbele ya uso wako, ziko furaha tele,

Na katika mkono wako wa kuume

Mkono wa kuume mna neema ya milele

Verse 5

Mungu nihifadhi mimi, maana nakukimbilia

Wewe Mungu wangu, Bwana ndiwe Bwana wangu,

Wewe Bwana ndiwe fungu la posho langu

Na la kikombe changu wewe unaishika kula yangu

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.