SectionsOffertorySadaka Yetu Bwana

Sadaka Yetu Bwana

Ordinary Time,MarianOffertory
Chorus

Sadaka yetu Bwana, twaomba upokee

Ni mazao ya mashamba yetu ee Baba upokee *2

Verse 2

Mkate na divai, na pia nafsi zetu

Ni zawadi yetu kwako, ee Baba upokee

Verse 3

Na fedha za mifukoni,mazao ya mashamba,

Ee Baba, kazi zetu, twaomba upokee(sadaka)

Verse 4

Pokea na nyoyo zetu, miili yetu pia

Ee Baba utupokee, tulio wana wako(sadaka)

Verse 5

Pokea tunakuomba, ingawa ni kidogo

Kwa unyenyekevu Baba, tunavileta kwako

Verse 6

Zawadi hii twaitoa, kwa sifa yako wewe,

Kwa ajili yetu sisi, nazo jamaa wetu (sadaka)

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.