Chorus
Sadaka yetu Bwana, twaomba upokee
Ni mazao ya mashamba yetu ee Baba upokee *2
Verse 2
Mkate na divai, na pia nafsi zetu
Ni zawadi yetu kwako, ee Baba upokee
Verse 3
Na fedha za mifukoni,mazao ya mashamba,
Ee Baba, kazi zetu, twaomba upokee(sadaka)
Verse 4
Pokea na nyoyo zetu, miili yetu pia
Ee Baba utupokee, tulio wana wako(sadaka)
Verse 5
Pokea tunakuomba, ingawa ni kidogo
Kwa unyenyekevu Baba, tunavileta kwako
Verse 6
Zawadi hii twaitoa, kwa sifa yako wewe,
Kwa ajili yetu sisi, nazo jamaa wetu (sadaka)
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.