Chorus
Sasa ni wakati mzuri twendeni madhabahuni,
Tukatoe sadaka zetu, tulijenge kanisa la Mungun{ Ewe ndugu yangu mkristu,
Changamka, changamka, peleka sadaka kwa Bwana.
Nenda katoe kwa moyo mweupe
Uzipate baraka za Mungu } *2
Verse 2
Mkristu kutoa sadaka,
Ndio wajibu wa kila mmoja,
Hivyo mkristu kumbuka wajibu,
Nenda katoe sadaka kwa Bwana.
Verse 3
Mwambie Bwana Mungu wako,
Baba pokea nilichokileta,
Hiki ndicho ulichonijalia,
Nakutolea kama shukrani.
Verse 4
Zamani za mababu zetu,
Walipeleka sadaka za nyama,
Nasi wakristu wa leo twendeni,
Tupeleke fedha za mifukoni.
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.