Chorus
{Siri ya moyo wangu, ni kilio changu
Na kilio cha moyo wangu, niione huruma yako } *2
Mungu wangu kinga yangu, nakuita Bwana
Ukinigeuka wewe nimekwisha mimi
Wewe ndiwe fimbo yangu, kimbilio langu
Ndiwe boma la wokovu, msaada wangu
Niepushie makucha ya dunia
Verse 2
Kikombe cha uchungu nimekunywa kwa harakwa
Sasa kimenikwama
Nimenaswa nimefikwa yamenikuta mimi
Ee Bwana ninakuita mimi ee Mungu njoo unikamilishe
Verse 3
Najua haina thamani, sala yangu ni chafu
Ibada haifai
Nimkimbilie nani zaidi yako wewe
Naililia huruma yako, mkono wako nishike Bwana
Verse 4
Mimi sistahili kabisa kupokea neema
Kutoka kwako Bwana
Ni mchafu ni mdhambi, nimeoza moyoni
Mikono nakuinulia Bwana, machozi yangu nafukia mimi
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.