SectionsExitSiri Ya Moyo Wangu

Siri Ya Moyo Wangu

Ordinary Time,MarianExit
Chorus

{Siri ya moyo wangu, ni kilio changu

Na kilio cha moyo wangu, niione huruma yako } *2

Mungu wangu kinga yangu, nakuita Bwana

Ukinigeuka wewe nimekwisha mimi

Wewe ndiwe fimbo yangu, kimbilio langu

Ndiwe boma la wokovu, msaada wangu

Niepushie makucha ya dunia

Verse 2

Kikombe cha uchungu nimekunywa kwa harakwa

Sasa kimenikwama

Nimenaswa nimefikwa yamenikuta mimi

Ee Bwana ninakuita mimi ee Mungu njoo unikamilishe

Verse 3

Najua haina thamani, sala yangu ni chafu

Ibada haifai

Nimkimbilie nani zaidi yako wewe

Naililia huruma yako, mkono wako nishike Bwana

Verse 4

Mimi sistahili kabisa kupokea neema

Kutoka kwako Bwana

Ni mchafu ni mdhambi, nimeoza moyoni

Mikono nakuinulia Bwana, machozi yangu nafukia mimi

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.