Sitawaacha nyinyi kama yatima,
Sitawaacha nyinyi (Acha nyinyi) asema
Bwana (ee Bwana) (Naja kwenu mioyonyenu ijae, furaha na amani,
Asema Bwana) *2 eeh
Nitawaombea nyinyi kwa Baba yangu
Naye atamtuma Roho wa kweli
Huyo Roho Baba atakayemtuma
Ndiye atakayewafariji mioyoni
Utukufu ulionipa ee Baba
Nimewapa na wao ili wapate
Kujua ndiwe peke uliyenituma
Ukawapenda wao ulivyonipenda
Baba hao ulionipa nataka
Wawe pamoja nami, nami popote
Popote kutazama utukufu wako
Utukufu ulionipa, anasema Bwana
Baba si hao tu ninawaombea
Lakini nao wale wataoniamini
Wote wawe umoja kama we Baba
Ulivyo ndani yangu nami ndani yako
Sitawaacha nyinyi kama yatima
Waipeleka roho, yako e Baba
Nawe unaufanya uso wa nchi
Uso wa nchi upya, anasema Bwana
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.