SectionsEntranceSote Tusimame

Sote Tusimame

Ordinary TimeEntrance
Chorus

Sote tusimame kwa heshima ya jina la Bwana

Tumwimbie Mungu wimbo mpya ule wa masifu

Kwa vinanda hata na vinubi tumwimbie

Mungu wetu aliyetuumba, ni Baba wa mababu zetu

Verse 2

Tupige vigelegele, tupigeni na makofi

Sisi tumekombolewa, tuimbe tushangilie

Verse 3

Kaigeuza bahari, ikawa nchi kavu,

Njooni tuyasimulie, matendo ya Mungu wetu

Verse 4

Alikemea bahari, mawimbi yakanyamaza

Mungu wetu ni mkuu, jina lake litukuzwe

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.