Verse 1
Tawi limechipuka shinani mwa Yesu
Kama tulivyopashwa habari na wazee
Likatoa ua, wakati wa usiku, lililochanua
Verse 2
Isaya alitaja ua hilo zuri
Ni Yesu mponya wetu, Maria alimzaa
Usiku mtulivu, uwezo wake Mungu, umefanya hivi
Verse 3
Na ua hili dogo lanuka vizuri
Lang'aa kama jua, giza lafukuza
Ni Mwana wa Mungu, hata mwana Adamu, Mwokozi wa watu
Verse 4
Siku ya kufa kwetu, Yesu tuongoze
Tuiache dunia, twende furahani
Mbinguni kwa Mungu, pale tutakusifu, milele daima
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.