SectionsExitTawi Limechipuka

Tawi Limechipuka

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,ChristmasExit
Verse 1

Tawi limechipuka shinani mwa Yesu

Kama tulivyopashwa habari na wazee

Likatoa ua, wakati wa usiku, lililochanua

Verse 2

Isaya alitaja ua hilo zuri

Ni Yesu mponya wetu, Maria alimzaa

Usiku mtulivu, uwezo wake Mungu, umefanya hivi

Verse 3

Na ua hili dogo lanuka vizuri

Lang'aa kama jua, giza lafukuza

Ni Mwana wa Mungu, hata mwana Adamu, Mwokozi wa watu

Verse 4

Siku ya kufa kwetu, Yesu tuongoze

Tuiache dunia, twende furahani

Mbinguni kwa Mungu, pale tutakusifu, milele daima

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.