Chorus
{ Tazama jinsi ilivyo vyema na kupendeza
Ndugu wakae pamoja, pamoja kwa umoja
Ndugu wakae pamoja kwa umoja } *2
Verse 2
Ni kama mafuta mazuri mazuri kichwani
Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni
Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake
Verse 3
Kama umande wa Hermoni, ushukao milimani pa Sayuni
Maana ndiko Bwana alipoamuru baraka naam uzima hata milele
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.