Tazama Mama mwanao, atundikwa msalabani
Sababu gani hi-yo, mwanao kutiwa hatianin{ Uchungu, mama, uchung,u mama,
Uchungu mama kwa mwanao } *2
[ s ] Sioni kosa lolote, alilolitenda mwanangu
Mwanangu hakuwa na kosa, makosa hayo juu yenu
Uchungu, uchungu, uchungu sana kwa mwanangu *2
[ t ] Kutundikwa juu msalabani, sababu yake ukombozi
Atukomboe utumwani, tuwe wana wa ukombozi
Ni sisi, ni sisi, ni sisi mama wakosefu *2
[ s ] Mwanangu haikumpasa, kufa bure bila sababu
Mwanangu Mungu mtu pekee, kwake sioni kosa kwangu
Uchungu, uchungu, uchungu sana kwa mwanangu *2
[ t ] Kumbuka mama Maria, maneno ya mwanao Yesu
Nitakufa nitafufuka, na kwenda juu kwa Baba yangu
Ya nini, ya nini, ya nini mama huzuni hiyo
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.