{Ee Bwana Mungu wangu
Tembea nami usiniache kwenye dunia (hiyo)
Ya machafuko } *2n
Nikianguka, Bwana, uniinue Bwana
Nikiteleza, Bwana, unishike mkono
Uniepushe na maadui wa roho yangu
Uniepushe na maadui wa roho yangu
Tazama ninaishi kwa mashaka na hofu kubwan(Kwani) Baadhi ya wanadamu wenzangu wamegeuka
Kuwa ni maadui zangu,
Wananiwinda wanikamate wavinyokoe viungo,
Eti wajipatie mali.
Tazama ninaishi kwa mashaka na hofu kubwan(Kwani) Baadhi ya waathirika wenzangu wamekamatwa
Bwana na wameshauawa,
Wamewakata vichwa na mikono, na miguu yao Bwana,
Eti wajipatie mali
Tazama sisi wanao wakiwa twakimbilia (kwako)n(Kwako) twazikabidhi roho zetu mikononi mwako
Maana ni wewe kimbilio
Usituachie adui zako watutie mikononi
Bwana utushike mkono
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.