Tuidhihirishe Imani

Ordinary Time,Advent,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Lent,Ordinary Time,Marian,Christmas,Ordinary Time,Ordinary TimePrayers of the Faithful
Chorus

Waamini tunaalikwa, kuidhihirisha imani yetu kwa matendon{Ni mwaliko wa Baba Mtakatifu, ni mwaliko wa Kanisa

Kuipa uhai imani tunayoikiri,nimani tunayoiadhimisha, imani tunayoiishi } * 2

Verse 2

Imani tunayoikiri,

Ndiyo kusadiki kwa Mungu mmoja mwumba Mbingu na nchi

Ndiyo kusadiki kwa Bwana mmoja Yesu Kristu

Ndiyo kusadiki kwa Roho Mtakatifu

Verse 3

Imani tunayoikiri,

Ndiyo kusadiki kwa kanisa moja takatifu Katoliki la mitume

Kuungama ubatizo mmoja, ufufuko wa wafu na uzima wa milele

Verse 4

Imani tunayoadhimisha, ndiyo sakramenti za kanisa

Zilizo chemichemi za neema tupatazo kwa Mungu

Sisi tunaomwamini Kristu na kumfuata

Verse 5

Imani tunayoiishi, ndiyo kuziweka maishani mwetu amri zote za Mungu

Bila kuyumbishwa na hisia za uhuru wa kidunia

Na kubaki katika mtazamo wa Kimungu kwa mafundisho ya kanisa

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.