Chorus
Tukuzeni Jina lake, milele na milele *2
Hubirini kwa watu ajabu zake zote
Semeni Bwana Mungu ni Bwana wa mabwanan{ Tangazeni kwa kuimba, kwa zaburi hata vinanda,
Na tarumbeta pia vinubi vyenye sauti ya kupendeza
Semeni ya kuwa ni Mfalme wa wafalme } *2
Verse 2
Mpeni Bwana utukufu,
Na nguvu pia mpeni, mwabuduni kwa uzuri wake,
Kwa uzuri wa utakatifu, tetemekeeni mbele zake
Verse 3
Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Mwimbieni Bwana wimbo mpya kwa maana ametenda
Ametenda mambo ya ajabu machoni pa mataifa
Verse 4
Paazeni sauti zenu,
Mkiimba kwa furaha, kwa madaha ukirukaruka
Ukicheza na kusimulia matendo yake ya ajabu
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.