SectionsExitTukuzeni Jina Lake

Tukuzeni Jina Lake

Ordinary Time,Ordinary TimeExit
Chorus

Tukuzeni Jina lake, milele na milele *2

Hubirini kwa watu ajabu zake zote

Semeni Bwana Mungu ni Bwana wa mabwanan{ Tangazeni kwa kuimba, kwa zaburi hata vinanda,

Na tarumbeta pia vinubi vyenye sauti ya kupendeza

Semeni ya kuwa ni Mfalme wa wafalme } *2

Verse 2

Mpeni Bwana utukufu,

Na nguvu pia mpeni, mwabuduni kwa uzuri wake,

Kwa uzuri wa utakatifu, tetemekeeni mbele zake

Verse 3

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,

Mwimbieni Bwana wimbo mpya kwa maana ametenda

Ametenda mambo ya ajabu machoni pa mataifa

Verse 4

Paazeni sauti zenu,

Mkiimba kwa furaha, kwa madaha ukirukaruka

Ukicheza na kusimulia matendo yake ya ajabu

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.