Chorus
Tumkimbie (tumkimbie) huyo huyo shetani (kimbia)
Shetani ameleta mafarakano katika dunia hii *2
Chuki zimetawala ee Bwana, magonjwa ni mengi sana
Tufanye nini tuepuke na matatizo haya *2
Verse 2
Tumeyasahau maagizo ya Bwana wetu Yesu Kristu
Aliyotufundisha sisi wanadamu, Ndiyo maana kuna machafuko
Verse 3
Mwenye masikio na ayasikilize maneno ya Bwana
Mkatende kama alivyotenda yeye, Dunia itakuwa na amani
Verse 4
Tungeishi na amani kama samaki katika bahari
Dunia hii ingekuwa ni paradise, Kama bustani ile ya Edeni
Verse 5
Tumelia sana Bwana hata machozi hayatoki tena
Tufanye nini sisi ni viumbe wako, Njoo haraka utusaidie
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.