SectionsExitTumkimbie Shetani

Tumkimbie Shetani

Ordinary TimeExit
Chorus

Tumkimbie (tumkimbie) huyo huyo shetani (kimbia)

Shetani ameleta mafarakano katika dunia hii *2

Chuki zimetawala ee Bwana, magonjwa ni mengi sana

Tufanye nini tuepuke na matatizo haya *2

Verse 2

Tumeyasahau maagizo ya Bwana wetu Yesu Kristu

Aliyotufundisha sisi wanadamu, Ndiyo maana kuna machafuko

Verse 3

Mwenye masikio na ayasikilize maneno ya Bwana

Mkatende kama alivyotenda yeye, Dunia itakuwa na amani

Verse 4

Tungeishi na amani kama samaki katika bahari

Dunia hii ingekuwa ni paradise, Kama bustani ile ya Edeni

Verse 5

Tumelia sana Bwana hata machozi hayatoki tena

Tufanye nini sisi ni viumbe wako, Njoo haraka utusaidie

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.