Verse 1
Twendeni kwa karamu ya Bwana tumeitwa
Twendeni twende kumpokea
Ni mwaliko wa Bwana
Tukale mkate wa uzima
Verse 2
Tujitakase mbele ya kwenda kwa karamu hii
Twendeni twende kumpokea
Twende watakatifu
Tukale mkate wa uzima
Verse 3
Karibu kwangu Yesu ukae kwangu daima
Twendeni twende kumpokea
Nifunze njia yako
Tukale mkate wa uzima
Verse 4
Na kwa uwezo wako imani yangu naikiri
Twendeni twende kumpokea
We-u Mungu Mwokozi
Tukale mkate wa uzima
Verse 5
Usituache basi pamoja nasi ukae
Twendeni twende kumpokea
Kwa kuwa kumekucha
Tukale mkate wa uzima
Verse 6
Na tufurahi mwisho pamwe na Baba milele
Twendeni twende kumpokea
Kwa umoja na Roho
Tukale mkate wa uzima
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.