Verse 1
{ Twendeni tuingie kwake
Na nyimbo nzuri za shangwe } *2
Verse 2
Dunia nzima imshangilie Bwana
Kwa furaha tumtumikie wote
Tumwendee na nyimbo za shangwe
Verse 3
Mjue Bwana wetu ni Mungu
Ametufanya na tuko watu wake
Sisi kondoo wa malisho yake
Verse 4
Ingieni mlangoni kwa kumsifu
Nyumbani mwake tumtolee heshima
Tutukuze jina lake kubwa mno
Verse 5
Kweli Mungu kwa Baba mwenyezi
Na kwa mwana Mwokozi wetu
Na kwa Roho Mtakatifu ndani mwetu
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.