Ufurahi moyo wao, wamtafutao Bwana *2n{ Mtafuteni Bwana, na nguvu zake
Utafuteni uso wake siku zote } *2
Kwa nyimbo nzuri na ngoma tamu, kwa vinubi pia vinanda,
Tupige makofi tumtukuze Mungu mwenye uwezo
Mshangilieni, mwimbieni Bwana
Usimulieni ukuu wake siku kwa siku
Simameni wababa wote, inukeni na kina mama
Vijana wacheze na watoto warukeruke leo
Msifuni Mungu, mwabuduni Yeye,
Tafuteni Bwana maana anapatikana
Lisifieni jina takatifu, nyanyukeni viumbe vyote
Zikumbukeni ajabu na hukumu ya kinywa chake
Msifuni Mungu, mwabuduni yeye
Mwambieni Yahweh, matendo yake yanatisha
Mshukuruni Mwenyezi Mungu, tangazeni ukuu wake
Yajulisheni mataifa mambo aliyoyatenda
Mshangilieni, mwambieni Bwana
Msimulieni matendo yake ya ajabu.
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.