SectionsExitUfurahi Moyo Wao (Ii)

Ufurahi Moyo Wao (Ii)

Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,MarianExit
Chorus

Ufurahi moyo wao, wamtafutao Bwana *2n{ Mtafuteni Bwana, na nguvu zake

Utafuteni uso wake siku zote } *2

Verse 2

Kwa nyimbo nzuri na ngoma tamu, kwa vinubi pia vinanda,

Tupige makofi tumtukuze Mungu mwenye uwezo

Mshangilieni, mwimbieni Bwana

Usimulieni ukuu wake siku kwa siku

Verse 3

Simameni wababa wote, inukeni na kina mama

Vijana wacheze na watoto warukeruke leo

Msifuni Mungu, mwabuduni Yeye,

Tafuteni Bwana maana anapatikana

Verse 4

Lisifieni jina takatifu, nyanyukeni viumbe vyote

Zikumbukeni ajabu na hukumu ya kinywa chake

Msifuni Mungu, mwabuduni yeye

Mwambieni Yahweh, matendo yake yanatisha

Verse 5

Mshukuruni Mwenyezi Mungu, tangazeni ukuu wake

Yajulisheni mataifa mambo aliyoyatenda

Mshangilieni, mwambieni Bwana

Msimulieni matendo yake ya ajabu.

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.