SectionsExitUhuru Wa Kweli

Uhuru Wa Kweli

Ordinary TimeExit
Verse 1

//utangulizin

Ninyi mliitwa ndugu muwe watu huru kabisa

Lakini uhuru huo sio wa kuusingizia

Isiwe ni sababu - ya kutawaliwa na tamaa hizi

Tamaa za dunia - msitawaliwe na tamaa za dunia

Ooh jifunzeni kutumikiana kwa upendo daima

Kwani sheria ni moja nayo ndiyo upendo

Chorus

n//kiitikio

Uhuru wangu ee - uhuru wangu

Uhuru wangu wa thamani

Uhuru wangu jamani - uhuru wangu (uhuru)

Unatokana na ukweli

Verse 3

Nikijisifu kwa uongo, nateseka

Kwani siwezi dhihirisha sifa yenyewe

Jamii itatarajia kutoka kwangu

Nisiyoweza kuyatenda, kwani si ya kweli!

Verse 4

Nikifanya udanganyifu, kwenye fedha

Nikimwona ausikaye ninazizima

Au nikipokea rushwa, nitanena

Hata yale yasiyo mema, yanidhalilishe!

Verse 5

Nikikosa uaminifu, kwenye ndoa

Nitakwepa kuongozana, na mpendwa wangu

Ili tusije kukutana, na hawara

Akashindwa kuvumilia, akanipondeza!

Verse 6

Nikizunguka nchi nzima, kuongea

Uwogo juu ya mwenzangu, najiumiza

Tukikutana ana njaa, yuko kimya

Nitadhani wamemwambia, nitapata hofu

Verse 7

Nikimtesa mpwa wangu, nimleaye

Sitatamani aonane na wazazi wake

Kwani najua atasema, nimtendeayo

Na mimi nitadhalilika, nitaaibika!

Verse 8

Nikifanya upendeleo, ofisini

Kumkweza asiyefaa, najidhihaki

Jamii ikimhubiri, afaaye

Nitahisi nakejeliwa na kuunguliwan

Verse 9

n// hitimishon---

Kwa sababu mimi, ndiye, ninaiandika mwenyewe

Historia yangu, leo, itakayosomwa milele

Daima milele, daima milele, daima milele

Muamuzi wangu ndimi!

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.