Chorus
Ujana ni maji ya moto bila Mungu ni majuto
Ujana ni maji ya moto ukicheza utakuchoma
Kunapokucha ni raga
Mwili bado una nguvu nyingi
Tunapomsahau Mungu vijana twapotea *2
Verse 2
Vishawishi ni vingi mno, ili tupate pesa nyingi
Wengine tunaua ili tupate pesa
Twaharibu amani ili tupate pesa
Tunapomsahau Mungu vijana twapotea
Verse 3
Magaidi wanatutumia, twauana sisi kwa sisi
Jamii inalia machozi ya uchungu
Wasio na hatia wauawa kwa nini
Tunapomsahau Mungu vijana twapotea
Verse 4
Ndoto zetu zinakatizwa, na wale wasio na utu
Wasiwasi kazini, wasiwasi shuleni
Mjini wasiwasi twatembea kwa hofu
Tunapomsahau Mungu vijana twapotea
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.