Verse 1
Hufanani nasi, unang'ara na tena una enzi, una utukufu
Umepita zote, sifa tunazokutolea sisi, nao malaika oho
Chorus
Wewe uko juu umetukuka na tunakuinua kwa nyimbo zetu hizi
Verse 3
Walikuimbia, baba zetu lakini hazikwisha, sifa zako wewe
Na watakatifu, wanaimba na hazimaliziki, tenzi hazitoshi oho
Verse 4
Mimea ya nchi, yaeleza inapopukutika, kuhifadhi maji
Kwamba wewe Bwana, hupungui unajua kuumba, hupitiwi neno oho
Verse 5
Kinyonga mdogo, anageuka rangi kujilinda, bila ya bunduki.
Anafafanua, umakini ndani ya kazi yako, isiyo dosari ohon
Verse 6
Na uhimidiwe, wewe Baba yaani ndiwe Mwana, Roho Mtukufu,
Ulivyotukuzwa, enzi zile sasa hata milele, utukuzwe pote ohon
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.