Uko Juu

Ordinary TimeExit
Verse 1

Hufanani nasi, unang'ara na tena una enzi, una utukufu

Umepita zote, sifa tunazokutolea sisi, nao malaika oho

Chorus

Wewe uko juu umetukuka na tunakuinua kwa nyimbo zetu hizi

Verse 3

Walikuimbia, baba zetu lakini hazikwisha, sifa zako wewe

Na watakatifu, wanaimba na hazimaliziki, tenzi hazitoshi oho

Verse 4

Mimea ya nchi, yaeleza inapopukutika, kuhifadhi maji

Kwamba wewe Bwana, hupungui unajua kuumba, hupitiwi neno oho

Verse 5

Kinyonga mdogo, anageuka rangi kujilinda, bila ya bunduki.

Anafafanua, umakini ndani ya kazi yako, isiyo dosari ohon

Verse 6

Na uhimidiwe, wewe Baba yaani ndiwe Mwana, Roho Mtukufu,

Ulivyotukuzwa, enzi zile sasa hata milele, utukuzwe pote ohon

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.