Chorus
{ Ewe mwenzangu univishe pete kwenye chanda changu,
Iwe ni alama ya uaminifu wako } *2
Verse 2
Naapa mbele ya Mungu, mimi ni wako siku zote,
Nitamuacha Baba nitamwacha na mama
Niambatane nawe, nasi tutakuwa mwili mmoja
Verse 3
Wewe sio malaika ni mwanadamu kama mimi,
Makosa kawaida tuko sawa maumbile
Maumbile ya Mungu, nitakusamehe ukinikosea
Verse 4
Macho yangu yameona, yameona wengi sana,
Kati yao wengi, ninakuvika pete
Iwe alama yangu ya uaminifu wangu kwako
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.