SectionsExitUpendo Na Ukarimu

Upendo Na Ukarimu

Ordinary Time,MarianExit
Verse 1

Watu wengi tunajaribu upendo

Tunawajali wale wanaotuhusu

Tunaojua wataweza kutulipa

Hatuwathamini wale wasiotuhusu

Wala wasiojiweza, lakini

Chorus

{Leo tumejifunza wote,nupendo ni kitu gani (wapendwa)

Tena tumepewa mfano,nukarimu una sifa gani (wapenzi) } * 2n

Verse 3

Tunawakopesha wenye kipato kikubwa

Tukiamini nao watatukopesha

Wakitujia wenye shida na fukara

Tunawakimbia eti hawakopesheki

Na wana madeni mengi, lakini

Verse 4

Wakiugua wenye nafasi za juu

Tunajazana kwao na vichupachupa

Tukiamini na sisi tukiugua

Watalundikana kwetu na vifuko fuko

Kadi na michango mingi, lakini

Verse 5

Tukitembelewa na mtu mwenye viraka

Tunauliza kama tulimualika

Akija aliyeshuka kwenye shangingi

Tunamwuliza kinywaji anachokunywa

Tena kwa unyenyekevu lakini

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.