Watu wengi tunajaribu upendo
Tunawajali wale wanaotuhusu
Tunaojua wataweza kutulipa
Hatuwathamini wale wasiotuhusu
Wala wasiojiweza, lakini
{Leo tumejifunza wote,nupendo ni kitu gani (wapendwa)
Tena tumepewa mfano,nukarimu una sifa gani (wapenzi) } * 2n
Tunawakopesha wenye kipato kikubwa
Tukiamini nao watatukopesha
Wakitujia wenye shida na fukara
Tunawakimbia eti hawakopesheki
Na wana madeni mengi, lakini
Wakiugua wenye nafasi za juu
Tunajazana kwao na vichupachupa
Tukiamini na sisi tukiugua
Watalundikana kwetu na vifuko fuko
Kadi na michango mingi, lakini
Tukitembelewa na mtu mwenye viraka
Tunauliza kama tulimualika
Akija aliyeshuka kwenye shangingi
Tunamwuliza kinywaji anachokunywa
Tena kwa unyenyekevu lakini
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.