SectionsThanksgivingUshuhuda Tosha

Ushuhuda Tosha

Ordinary TimeThanksgiving
Verse 1

Tuna haki ya kutamka na kutoa ushuhuda

Mambo mema alotenda Mungu pia na kwa huruma

Ninamwambia naye jirani Mungu ana huruma

Chorus

{ Ushuhuda, huo ni ushuhuda tosha (nasema)

Ni huruma, Mungu ana huruma nyingi (hakika)

Ninapolala pia ninaamka huo wote ni ushuhuda tosha } *2

Verse 3

Kaumba mbingu na dunia wanyama hata samaki

Binadamu na akili nyingi sisi tukawatawale

Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu

Verse 4

Tunalala bila kuomba hatimaye twaamka

Mungu wetu na hakasiriki bado atupa mkate

Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu

Verse 5

Maisha yetu twayapanga nayo yanafanikiwa

Mara nyingi hata hatuombi kumshirikisha Mungu

Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu

Verse 6

Tunapofanya biashara uongo tunatumia

Twazikiuka amri za Mungu ili tupate faida

Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu

Verse 7

Ni mengi hatujatamka wanadamu tunafanya

Tunaomba msamaha Mungu sisi sote walegevu

Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.