Verse 1
Utukufu kwa Mungu Baba juu mbingunin
Chorus
Utukufu kwa Mungu juu mbinguni na amani
Amani duniani kwa watu wenye mapenzi mema
Verse 3
Nayo sifa na heshima tunakupa wewe
Na ibada, utukufu pia kwako wewe
Verse 4
Ewe Bwana ndiwe mfalme juu mbinguni
Bwana Mungu Baba, Baba mwenyezi
Verse 5
Ewe Bwana ndiwe mfalme juu mbinguni
Bwana Mungu mwana kondoo wa Mungu Bwana
Verse 6
Ewe mwenye kuondoa dhambi za dunia
Twakuomba ee Bwana utuhurumie
Verse 7
Ewe mwenye kuondoa dhambi za dunia
Twakuomba upokee ombi letu Bwana
Verse 8
Ewe mwenye kuketi kule kuume
Kuume kwa Mungu Baba utuhurumien
Verse 9
Peke yako mtakatifu, peke yako Bwana
Peke yako u mkuu Yesu Kristu
Verse 10
Pamoja naye Roho, Roho Mtakatifu
Katika utukufu wake Mungu Baba
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.