SectionsEucharistUtukufu (Migori)

Utukufu (Migori)

Ordinary Time,MarianEucharist
Chorus

Utukufu kwa Mungu juu

Na amani duniani

Na amani kwa watu woten{Wenye - wenye mapenzi,

Watu - wenye mapenzi

Mema - wenye mapenzi

Watu - wenye mapenzi mema }*2

Verse 2

Tunakusifu tunakuheshimu

Tunakuabudu tunakutukuza

Tunakushukuru kwa ajili ya

Utukufu wako, wako mkuu

Verse 3

Ee Bwana Mungu mfalme wa mbinguni,

Mungu Baba mwenyezi ee Bwana Yesu Kristu

Mwana wa pekee ee mwana Mungu

Mwanakondoo wa Mungu, mwana wa Baba

Verse 4

Mwenye kuondoa dhambi za dunia

Ewe mwenye kuondoa dhambi za dunia

Pokea ombi letu ewe mwenye kuketi

Kuume kwa Baba, utuhurumien

Verse 5

Kwa kuwa ndiwe uliye peke yako

Peke yako mkuu ee Bwana Yesu Kristu

Pamoja na roho mtakatifu

Katika utukufu, wa Mungu Baba amina

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.