SectionsOffertoryUtukuzwe Ewe Bwana

Utukuzwe Ewe Bwana

Ordinary Time,MarianOffertory
Verse 1

Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe, aleluya

Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe, aleluya

Chorus

Utukuzwe - utukuzwe

Baba Muumba ulimwengu - aleluya

Verse 3

Tumepokea mkate, mazao ya mashamba, aleluya

Ndio alama kwetu, ya wema wako mkuu, aleluya

Verse 4

Ni tunda la bidii, ya mkono na ya moyo, aleluya

Jalie uwe kwetu, chakula cha uzima, aleluya

Verse 5

Zawadi ya divai, kutoka mzabibu, aleluya

Ndiyo alama kwetu, ya wema wako mkuu, aleluya

Verse 6

Ni tunda la bidii, ya mkono na ya moyo, aleluya

Jalie iwe kwetu, kinywaji cha kiroho, aleluya

Verse 7

Sifa kwako ee Mungu uliyetuchagua, aleluya

Shukrani kwako Baba, kwa kutulisha sisi, aleluya

Verse 8

Kwa pendo na fadhili, umetufurahisha, aleluya

Ukatufikisha kwa sherehe yetu leo, aleluya

Verse 9

Siku ya leo iwe kwa heshima na sifa, aleluya

Na utukufu wako na kwa mafaa yako, aleluya

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.