Chorus
Uzuio wa umeme, mlinzi wa Kimasai
Mbwa mkali tunguri na silaha za kisasanhakika, hazifai kitu, kweli hazifai kitu
Bwana amtumapo mjumbe kuchukua roho yako
Verse 2
Wako wapi, wako wapi waliowahi kutikisa dunia?
Wako wapi walioita miungu na dunia?
Na hakuna hata mmoja wao aliyewahi kujikinga
Bwana alipomtuma mjumbe kumchukua?
Verse 3
Wako wapi, wako wapi waliowahi kuishi angani?
Wako walio ishi kwenye madaha?
Je hakuna hata mmoja wao aliyeweza kujificha
Bwana alipomtuma mjumbe kumchukua
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.