Chorus
Viuzeni mlivyo navyo mtoe sadaka
Kwani mnajiwekea hazina mbinguni
Verse 2
Ziwekeni fedha zenu katika akiba ya mbinguni
Ziwekeni mali zenu katika mifuko ya mbinguni
Verse 3
Msidhani kwamba mnazipoteza mali zenu bure
Kweli kwamba mnaweka katika hazina ya mbinguni
Verse 4
Viuzeni mali zenu mtoe sadaka kwake Bwana
Viuzeni vitu vyote mweke hazina ya mbinguni
Verse 5
Rudisheni vitu vyote kwani yeye ndiye aliwapa
Aliwapa bure nanyi pia mkazirudishe bure
Verse 6
Mkatoe kwake Bwana kwa moyo mmoja na mapendo
Ni akiba mnaweka katika mifuko ya mbinguni
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.