SectionsExitZanena Siku Kuu

Zanena Siku Kuu

ChristmasExit
Verse 1

Zanena, siku kuu,

Kengele za juu,

Waumini furahini,

Mkombozi mkumbusheni

Mzawa leo Bethlehemu

Mzawa leo Bethlehemu

Verse 2

Ni hii leo, siku heri,

Siku nzuri nzuri,

Ya uasi kuondolewa,

Ya mbingu kufunguliwa

Yakisha maulaumu,

Yakisha malaumu

Verse 3

Ni hii leo, siku njema,

Siku ya salama,

Aliposhuka Mwokozi,

Mwanaye Mungu Mwenyezi

Kuwa mwanadamu,

Kuwa mwanadamun

Verse 4

Leo siku, hakika,

Wala hamna shaka

Kwamba dhambi ya asili,

Yaweza kufutwa kweli

Ina dawa timamu,

Ina dawa timamun

Verse 5

Leo siku ya neema,

Yameshuka mema

Asifiwe Mungu juu,

Watu wa imani kuu

Waletewa amani,

Waletewa amani

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.