Verse 1
Zanena, siku kuu,
Kengele za juu,
Waumini furahini,
Mkombozi mkumbusheni
Mzawa leo Bethlehemu
Mzawa leo Bethlehemu
Verse 2
Ni hii leo, siku heri,
Siku nzuri nzuri,
Ya uasi kuondolewa,
Ya mbingu kufunguliwa
Yakisha maulaumu,
Yakisha malaumu
Verse 3
Ni hii leo, siku njema,
Siku ya salama,
Aliposhuka Mwokozi,
Mwanaye Mungu Mwenyezi
Kuwa mwanadamu,
Kuwa mwanadamun
Verse 4
Leo siku, hakika,
Wala hamna shaka
Kwamba dhambi ya asili,
Yaweza kufutwa kweli
Ina dawa timamu,
Ina dawa timamun
Verse 5
Leo siku ya neema,
Yameshuka mema
Asifiwe Mungu juu,
Watu wa imani kuu
Waletewa amani,
Waletewa amani
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.