Zawadi Tosha

Ordinary Time,MarianThanksgiving
Chorus

Nimetunukiwa tuzo lenye thamani

Nimeletewa zawadi toka mbinguni

Nimejishindia Mwana wa Mungu

Nimepewa Yesu zawadi tosha

Verse 2

Ninashangilia naimba kwa furaha

Ninarukaruka nacheza kwa furaha

Napiga makofi na vigelegele

Nimempata Yesu tuzo la ajabu (mimi)

Verse 3

Ninakushukuru ee Mungu Baba yetu

Nasema asante kwa mema yako yote

Napiga filimbi, ngoma na kayamba

Nimejishindia Bwana wa mabwana

Verse 4

Nikiwa na Yesu, magonjwa yamepona

Nikiwa na Yesu mashaka yamekwisha

Yesu kiongozi, Yesu Jemedari

Yesu mchungaji, Yesu mambo yote

Verse 5

Maisha marefu ni tuzo nimetuzwa

Uzima milele nimeshaahidiwa

Mbinguni kwa Baba nitakaribishwa

Nitaishi vyema siku zangu zote

Comments

Sign in to join the conversation

Share your thoughts on this hymn with the community.