Zawadi Tosha
Ordinary Time,MarianThanksgiving
Chorus
Nimetunukiwa tuzo lenye thamani
Nimeletewa zawadi toka mbinguni
Nimejishindia Mwana wa Mungu
Nimepewa Yesu zawadi tosha
Verse 2
Ninashangilia naimba kwa furaha
Ninarukaruka nacheza kwa furaha
Napiga makofi na vigelegele
Nimempata Yesu tuzo la ajabu (mimi)
Verse 3
Ninakushukuru ee Mungu Baba yetu
Nasema asante kwa mema yako yote
Napiga filimbi, ngoma na kayamba
Nimejishindia Bwana wa mabwana
Verse 4
Nikiwa na Yesu, magonjwa yamepona
Nikiwa na Yesu mashaka yamekwisha
Yesu kiongozi, Yesu Jemedari
Yesu mchungaji, Yesu mambo yote
Verse 5
Maisha marefu ni tuzo nimetuzwa
Uzima milele nimeshaahidiwa
Mbinguni kwa Baba nitakaribishwa
Nitaishi vyema siku zangu zote
Comments
Sign in to join the conversation
Share your thoughts on this hymn with the community.